---
1. UTI (Maambukizi ya Njia ya Mkojo)
UTI (Urinary Tract Infection) ni maambukizi yanayotokea kwenye mfumo wa mkojo, hasa kibofu na mrija wa mkojo (urethra). Wanawake wako kwenye hatari zaidi ya kupata UTI kuliko wanaume.
Dalili za UTI
Maumivu au hisia ya kuwashwa wakati wa kukojoa
Haja ya kukojoa mara kwa mara
Mkojo wenye harufu mbaya au wenye rangi isiyo ya kawaida
Maumivu ya tumbo au sehemu ya chini ya mgongo
Sababu za UTI
Bakteria (hasa E. coli) wanaoingia kwenye njia ya mkojo
Kushindwa kukojoa mara kwa mara
Kutumia choo kichafu
Mahusiano ya kimapenzi bila kujilinda
Matibabu na Kinga
Kunywa maji mengi kusaidia kusafisha njia ya mkojo
Kutumia antibiotics zilizopendekezwa na daktari
Kuepuka kubana mkojo kwa muda mrefu
Kujisafisha vizuri baada ya kutumia choo
Comments
Post a Comment