KISUKALI (DM): Aina, Dalili, Sababu, na Namna ya Kudhibiti
Maana ya KISUKALI
Ugojwa wa kisukali (DM) ni kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili unavyotumia sukari (glucose). Glucose ni chanzo kikuu cha nishati kwa mwili, lakini kwa wagonjwa wa DM, kuna tatizo katika kuzalisha au kutumia insulini, homoni inayodhibiti kiwango cha sukari mwilini.
Aina za kisukali
1. Kisukali Aina 1 – Mwili hausambazi insulini kabisa. Mara nyingi huwapata watoto na vijana.
2. Kisukali aina 2 – Mwili hautumii insulini ipasavyo. Ni aina ya kawaida zaidi na mara nyingi huhusiana na maisha duni ya lishe na uzito mkubwa.
3. Kisukali cha Mimba – Huwaathiri wanawake wajawazito lakini hupotea baada ya kujifungua.
Dalili za Kisukali
Kiu kupita kiasi
Kukojoa mara kwa mara
Kupungua uzito bila sababu
Uchovu mwingi
Maambukizi ya mara kwa mara, hasa kwenye ngozi na sehemu za siri
Sababu za Kisukari
Urithi wa vinasaba (Genetics)
Mtindo wa maisha duni (Lishe mbaya na kutokufanya mazoezi)
Uzito mkubwa wa mwili (Obesity)
Matatizo ya mfumo wa kinga kwa Aina 1 Ya kisukali
Njia za Kudhibiti na Kutibu kisukali
Kula chakula bora chenye wanga kidogo
Kufanya mazoezi mara kwa mara
Kudhibiti uzito wa mwili
Kutumia dawa kama insulini (kwa wenye Type 1) au vidonge vya kisukari
Kufuatilia kiwango cha sukari kwa kutumia glucometer
Matibabu ya kisukali ni pamoja na kutumia dawa za hospitali kwa usahihi kabsa ikiwemo insulin na zile za vidonge kama metformin
Comments
Post a Comment